Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akifuatilia
hotuba ya Makamu wa Rais wa Nigeria, Mhe Kashim Shettima (Hayupo pichani)
wakati akifungua Mkutano wa 24 wa Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za
nchi za Afrika ambazo ni Wanachama wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la
Kimataifa (IMF) (Africa Caucus Meetings) unaofanyika katika Hoteli ya Transcorp
Hilton, mjini Abuja Nchini Nigeria, ambao unajadili namna ya kuboresha biashara
katika nchi za Afrika kwa kuweka mazingira mazuri ya kusisimua biashara kwa
kujenga miundombinu itakayowezesha kukuza biashara miongoni mwa nchi za Afrika
na wataweka msimamo wa pamoja na kupeleka agenda ya namna Taasisi za Fedha za Kimataifa ikiwemo Benki
ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, zinatakiwa kuziwezesha nchi hizo
kifedha na kiutaalam ili zifikie malengo husika.
......................................
Na Benny Mwaipaja
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 24 wa Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za nchi za Afrika ambazo ni Wanachama wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) (Africa Caucus Meetings) unaofanyika katika Hoteli ya Transcorp Hilton, mjini Abuja Nchini Nigeria. Mkutano huo umefunguliwa rasmi tarehe 2 Agosti, 2024 na Makamu wa Rais wa Nigeria, Mhe Kashim Shettima.
Mkutano huo unajadili namna ya kuboresha biashara katika nchi za Afrika kwa kuweka mazingira mazuri ya kusisimua biashara kwa kujenga miundombinu itakayowezesha kukuza biashara miongoni mwa nchi za Afrika na wataweka msimamo wa pamoja na kupeleka agenda ya namna Taasisi za Fedha za Kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, zinatakiwa kuziwezesha nchi hizo kifedha na kiutaalam ili zifikie malengo husika.


Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), (wa tatu
kushoto-nyuma), akiwa katika picha ya pamoja ya Mawaziri wa Fedha wa nchi za
Afrika wakiwa na Makamu wa Rais wa Nigeria, Mhe. Kashim Shetima (mwenye vazi
jeupe-mbele), baada ya hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa 24 wa Mawaziri wa Fedha
na Magavana wa Benki Kuu za nchi za Afrika ambazo ni Wanachama wa Benki ya
Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) (Africa Caucus Meetings)
unaofanyika katika Hoteli ya Transcorp Hilton, mjini Abuja Nchini Nigeria,
ambao unajadili namna ya kuboresha biashara katika nchi za Afrika kwa kuweka
mazingira mazuri ya kusisimua biashara kwa kujenga miundombinu itakayowezesha
kukuza biashara miongoni mwa nchi za Afrika na wataweka msimamo wa pamoja na
kupeleka agenda ya namna Taasisi za
Fedha za Kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF,
zinatakiwa kuziwezesha nchi hizo kifedha na kiutaalam ili zifikie malengo
husika.
No comments:
Post a Comment