ZIPA YAKUTANA NA UJUMBE KUTOKA CBE KUJADILI UJENZI WA CHUO CHA BIASHARA ZANZIBAR - UMOJA BANKING BLOG

Home Top Ad

MABENK

Post Top Ad

Saturday, 13 July 2024

demo-image

ZIPA YAKUTANA NA UJUMBE KUTOKA CBE KUJADILI UJENZI WA CHUO CHA BIASHARA ZANZIBAR

Untitled-2

 

1

Mkurugenzi ZIPA , Saleh Saad Mohamed

.............................

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

MAMLAKA ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) imekutana na Ujumbe kutoka Chuo cha Biashara CBE kwa majadiliano na maandalizi ya ujenzi wa Chuo hicho hapa Zanzibar katika maeneo huru ya Uwekezaji Fumba.

Akizungumza na Ujumbe huo Ofisini kwake ZIPA Maruhubi Mkurugenzi ZIPA , Saleh Saad Mohamed amesema Uwekezaji huo hapa Zanzibar utaondoa usumbufu kwa Wazanzibar watakaotaka kujifunza, sambamba na kuwapunguzia gharama za masomo.

Mkurugenzi Saleh amesema CBE na ZIPA wanaweza kufanya kazi kwa pamoja kutokana na ufanano wa mahitaji yao kiutendaji na kitaaluma kutokana CBE ni Chuo cha Biashara na ZIPA inatoa huduma za Uwekezaji na Taaluma yake.

Amesema ZIPA ili iendane na kasi ya mabadiliko ya kiteknolojia yanayoikumba dunia ni lazima watumishi wake wapatiwe mafunzo ya mara kwa mara ili kukabiliana na mabadiliko hayo.

Nae Mkuu wa Chuo Prof. Tandi Lwoga amesema CBE itayafanyia kazi yale yote yaliyopendekezwa na Mkurugenzi ikiwemo suala zima la mafunzo kwa watumishi wa ZIPA.

CBE inatarajia kujenga majengo yake hapa Zanzibar tu taratibu za Uwekezaji kwa Chuo hicho utakapokamilika.2Mkurugenzi ZIPA , Saleh Saad Mohamed (kulia), akizungumza na ujumbe kutoka Chuo cha Biashara CBE) kuhusu ujenzi wa hicho utakao fanyika maeneo  huru ya Uwekezaji Fumba.  Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages

undefined

Contact Form

Name

Email *

Message *