BENKI YA NMB YATOA ELIMU YA MATUMIZI BORA YA FEDHA KWA WALIMU MAKAMBAKO NJOMBE - UMOJA BANKING BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, 17 July 2024

BENKI YA NMB YATOA ELIMU YA MATUMIZI BORA YA FEDHA KWA WALIMU MAKAMBAKO NJOMBE


 Baadhi ya walimu wa Halmashauri ya Mji wa Makambako Mkoa wa Njombe wakiwa kwenye mafunzo ya matumizi bora ya fedha. Mafunzo hayo yamewezeshwa na ,Mkurugenzi wa  halmashauri ya mji wa Makambako kwa kushirikiana na Benki ya NMB..

...............................

Na Mwandishi Wetu, Njombe

NJOMBE, Baada ya kuona kundi kubwa la walimu wamejiingiza kwenye mikopo umiza na kuathiri utekelezaji wa majukumu yao ya ufundishaji ,Mkurugenzi wa  halmashauri ya mji wa Makambako kwa kushirikiana na benki ya NMB imetoa elimu ya fedha na mikopo kwa njia ya mfumo wa PEPMIS ili kuepusha usumbufu na mikopo. 

Wakati Wakifungua mafunzo ya mikopo na matumizi ya fedha yalioandaliwa na NMB kwa walimu wa shule za msingi na sekondari ,Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Wakambako Keneth Haule na Hamza Mandwanga wamesema walimu wanapaswa kuachana na tabia ya kuchukua mikopo mitaani na kutumbukia kwenye matatizo makubwa na kuwaondol 

Awali meneja mwandamizi NMB Makao Maku Ally Ngingite na Straton Chilongola meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu kusini wamesema baada ya kutambua changamoto zinazoikumba kada ya walimu na wakalazimika kuja na suluhisho la kifurushi cha walimu chenye huduma nyingi za kifedha ikiwemo mikopo kidigitali na kisha Edfonce Mbasha akaeleza manufaa ya mikopo ya kilimo kwa wlaimu. 

Kwa upande wao wanufaika wa mafunzo hayo akiwemo Shaban Ambindwile wamesema elimu ya fedha na uombaji wa mikopo kupitia mfumo wa kielektronic wa PEPMIS utawasaidia kujiepusha na mikopo umiza na kausha dani wanayochukua mitaani na kuishia kwenye matatizo.

Baada kutoa elimu ya fedha na mikopo kwa walimu kupitia mfumo wa PEPMIS ,NMB inakusudia kukutana na walimu wengine kutoka mikoa ya Mbeya na Mkasi Katavi ili kuwakomboa kwenye changamoto hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages