BOT YATOA ELIMU YA UTAMBUZI WA NOTI BANDIA KWA WANAFUNZI MKOANI TANGA - UMOJA BANKING BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, 22 January 2026

BOT YATOA ELIMU YA UTAMBUZI WA NOTI BANDIA KWA WANAFUNZI MKOANI TANGA

Mchambuzi wa Masuala ya Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Charles Kanuda, akizungumza na waandishi wa habari Januari 22, 2026 katika Maadhimisho ya Wiki ya Fedha Kitaifa yanayoendelea Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga.

................................. 

Na Mwandishi Wetu,Tanga.


BENKI Kuu ya Tanzania (BOT) imetoa elimu ya utambuzi wa noti bandia kwa Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mkwakwani mkoani Tanga.


Mwanafunzi wa darasa la sita wa Shule hiyo, Adrus Mahmoud  akizungumza na waandishi wa habari Januari 22, 2026 wakati  walipotembea banda la benki hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Fedha Kitaifa yanayoendelea Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga aliishukuru benki hiyo kwa elimu waliyopewa.


“Tunaishukuru BoT kwa elimu  ambayo imetupatia na sisi kwa niaba ya wenzetu ambao hawakubatika kufika katikakatika maadhimisho haya tutakwenda kuwapa,” alisema Mahmoud.


Alisema amefarijika amefarijika kupatiwa elimu ya ziada juu ya kutambua alama za kificho zilizomo kwenye noti ambayo itawasaidia kuzibaini wakiwa nyumbani kwao na maeneo mengine.


Mwalimu wa shule hiyo, Mwajuma Kileo alisema elimu hiyo inakwenda kuwasaidia wanafunzi na kuwa mabalozi kwa wenzao ambao hawakuwepo kwenye ziara hiyo ya mafunzo.


Wakati huohuo Afisa Mwandamizi Mkuu kutoka Kurugenzi ya Usimamizi wa Sekta ya Fedha wa benki hiyo, Mwile Kauzeni, mewataka watu wanaojihusisha na biashara ya kubadilisha fedha za kigeni bila ya kuwa na leseni kuacha mara moja kwani wanatenda kosa la jinai.


“Tunawaagiza watu wote wanaojihusisha na biashara hiyo kinyume na utaratibu wafuate sheria ili waweze kufanya kazi hiyo kwa halali kinyume na hapo wanaikosesha serikali mapato,”  alisema Kauzeni.


Kauzeni aliwataka wote wanaofanya biashara hiyo kutembelea matawi ya benki hiyo ili kujua taratibu za kujisajili au kupitia mtandao wa benki hiyo.


Kwa upande wake Mchambuzi wa Masuala ya Fedha wa benki hiyo , Charles Kanuda alisema Serikali imeanzisha mfuko wa udhamini wa mikopo na kwa mtanzania ambaye atahitaji lakini hana dhamana atapatiwa dhamana mpaka asilimia 75.


Alisema watu wengi wamekuwa wakijaribu kwenda kukopa huku wakiombwa dhamana yenye thamani kubwa zaidi ya mikopo wanayohitaji hivyo kushindwa kupata mikopo.


Alisema baadhi ya watu wameshindwa kuchukua mikopo au kuchukua kiasi kidogo jambo ambalo limeathiri ufanisi wa biashara zao wanazoziendesha.


Kauli Mbiu ya maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Wizara ya Fedha ni “Elimu ya fedha , msingi wa Maendeleo ya kijamii na kiuchumi" 

Meneja Msaidizi Sarafu, Joyce Saidimu kutoka Arusha, akiwakabidhi vipeperushi wanafunzi wa shule hiyo.
Afisa Mwandamizi Mkuu kutoka Kurugenzi ya Usimamizi wa Sekta ya Fedha wa benki hiyo, Mwile Kauzeni akizungumza na waandishi wa habari kwenye maadhimisho hayo.
Mwanafunzi wa darasa la sita wa Shule hiyo, Adrus Mahmoud  akizungumza na waandishi wa habari
Mwalimu wa shule hiyo, Mwajuma Kileo akizungumzia ziara hiyo ya mafunzo.
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages