Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Magharibi (TMA) Bw. Elias Elipiki, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa maafisa ugani yaliyotolewa na TMA kwa kushirikiana na Benki ya CRDB kupitia mradi wa Tanzania Agriculture Climate Adaptation Technology Deployment Project (TACATDP).
.................................................
Na Mwandishi Wetu, Mbeya
Wataalamu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) kwa kushirikiana na
Benki ya CRDB kupitia mradi wa Tanzania Agriculture Climate Adaptation
Technology Deployment Project (TACATDP) wamewajengea uwezo Maafisa Ugani wa
namna bora ya kutafsiri na kutumia taarifa za hali ya hewa hususani katika
shughuli za kilimo.
Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo Meneja wa Kanda ya
Nyanda za Juu Kusini Magharibi (TMA) Bw. Elias Elipiki, alisema mafunzo hayo
yanawalenga Maafisa Ugani kwani wao ni daraja kati ya TMA na wakulima, hivyo
mafunzo haya yanalenga kutoa elimu ya namna sahihi ya kutafsiri taarifa
za hali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka na kuwawezesha wakulima kufanya mipango
sahihi juu ya shughuli za kilimo kwa msimu husika.
Aidha, Meneja Uhusiano kutoka CRDB ambaye pia ni msimamizi wa
utoaji wa mikopo inayozingatiwa uhifadhi wa mazingira katika mradi wa (TACATDP)
Bw. Karim Kindole, alisema CRDB na TMA wana ushirikiano katika kuwajengea
uwezo Maafisa Ugani namna ya kudhibiti na kuwasaidia wakulima kupata taarifa sahihi
za mabadiliko ya hali ya hewa.
Naye, Afisa Kilimo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Bw.
Sostenesi Silayo, aliwashukuru TMA na CRDB kwa kuwapa nafasi Maafisa Ugani
kupata elimu ambayo wataitumia katika kuwashauri wakulima kulima kilimo sahihi
kutokana na hali ya hewa husika na kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao
mengi.
Mafunzo kwa vitendo yakiendelea kutolewa kwa maafisa ugani hao.
Meneja Uhusiano kutoka CRDB ambaye pia ni msimamizi wa utoaji wa mikopo inayozingatiwa uhifadhi wa mazingira katika mradi wa (TACATDP) Bw. Karim Kindole, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo.Mafunzo kwa vitendo yakitolewa.
Mafunzo yakiendelea.
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wanaotekeleza mradi huo.
No comments:
Post a Comment