Akifafanua, Shipela alisema wakati Mkulima atapata bei bora na yenye uwiano, uhakika wa soko, kuamsha ari na hamasa ya uboreshaji wa kakao na kuongeza kipato, Serikali za Mitaa na Serikali Kuu nazo zitanufaika kwa kuongeza kipato, kukuza na kuendeleza uzalishaji zao, Kodi ya Thamani (VAT) na PAY E na ajira kwa vijanana wanawake.
Kaimu Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika Wilaya ya Kyela (KYECU Ltd), Nabii Emmanuel Mwakyenda, aliishukuru NMB Foundation kwa kuwapiga msasa wanachama wa AMCOS 37 za wilaya yake, akiamini mafunzo na elimu waliyopata itakuwa chachu ya ustawi na uendelevu wa Kakao wilayani humo.
Akisoma risala kwa niaba ya washiriki, Evance Mwaipopo kutoka Mwabusye AMCOS, aliipongeza NMB Foundation kwa uendeshaji wa mafunzo, ambayo yamewamenufaisha kupitia mada mbalimbali zikiwamo za Uongezaji Thamani wa Kakao, Kilimo cha Kakao Bila Kukata Miti na Ujasiriamali na Mpango Biashara.
Washiriki wakaiomba NMB Foundation kuendelea kuwajali na kuwathamini wakulima wa kakao Kyela, huku wakiitaka Serikali kwa upande wake izitupie macho barabara zinazoingia na kutoka Kyela, ambazo ni chakavu, ili kurahisisha usafirishaji wa mazao mbalimbali, ikiwemo kakao.
No comments:
Post a Comment