BENKI YA CRDB YATAJWA KUWA NI MOJA YA TAASISI ZINAZOLIPA KODI VIZURI KWA MWAKA 2023/ 2024 - UMOJA BANKING BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, 23 January 2025

BENKI YA CRDB YATAJWA KUWA NI MOJA YA TAASISI ZINAZOLIPA KODI VIZURI KWA MWAKA 2023/ 2024

Benki ya CRDB imetangazwa kuwa moja ya taasisi zinazolipa kodi zilizofanya vizuri zaidi kwa mwaka 2023/2024 katika tuzo za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) zinazotolewa usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa The Super Dome Masaki ambapo Mgeni Rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Tuzo hiyo imepokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alieambata na Afisa Mkuu wa Fedha, Fredrick Nshekanabo. Tuzo hii ni muendelezo wa kutambuliwa kwa benki ndani na nje ya nchi ambapo kwa mwaka 2024, Benki ya CRDB imepata tuzo zaidi ya 50 katika nyanja mbalimbali.

 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages