I
Na Mwandishi Wetu
BENKI ya I&M ikiwa katika
kusherehekea kutimiza miaka 50 ya utendaji kazi na ufanisi, imeanzisha huduma
ya kisasa ya Rafiki Chat Banking iliyoboreshwa ili kuwarahisishia huduma wateja
wao, huduma hiyo ambayo inapatikana kupitia WhatsApp itakuwa inarahisisha
utoaji wa huduma mbalimbali za kibenki ikiwa ni pamoja na kuangalia salio la
akaunti papo kwa papo, kupokea taarifa za miamala pamoja na kuhamisha au kutuma
fedha kirahisi.
Hayo na yamebainishwa na Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo Zahid Mustafa wakati
akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ikiwa ni katika
uzinduzi huduma hiyo, huku akibainisha kuwa, benki hiyo inaendelea kufanya
ubunifu kwa mustakabali endelevu na kuunga mkono mabadiliko ya kidijitali
nchini.
“Sisi kama I&M sio tu kwamba hii ni bidhaa yetu ya kwanza bali tupo
tunajikita zaidi kwenye dhamira kuingia kwenye ulimwengu wa kidijitali lakini
pia tumeingia ushirikiano na Airtel inaitwa kamilisha ambapo tunaweza kuwafikia
watanzania wengi zaidi na kuwapa huduma bora zaidi,” amesema Mustafa.
Mtendaji mkuu huyo, amesema dhamira yao ni kuhakikisha wanaondoa matumizi
ya karatasi kwenye utoaji huduma kwa wateja wake na badala yake kila kitu
kitakuwa kinafanyika kwa njia ya kidigitali ikiwa pia ni sehemu ya kuunga mkono
ama kuchangia Dira ya serikali ya Tanzania ya uchumi wa kidijitali chini ya
uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.
Naye Mkuu wa Kitengo cha wateja Rejareja katika benki hiyo Simon Gachachi
amesema kuwa wamekusudia kuwekeza katika kujenga utendaji zaidi na vipengele
vinavyofanya kazi kwa washirika wao wa teknolojia, ambapo pia katika kuboresha
zaidi huduma hiyo, amesema mwezi Septemba watazindua namna mteja ataweza kulipa
kodi na malipo mengine ya serikali kupitia WhatsApp kwa kutumia mifumo
mbalimbali.
Kwa upande wake Meneja wa bidhaa za kidijitali wa benki hiyo Adam Emmanuel
ameeleza kuwa huduma hiyo walianzisha tangu mwaka 2021 ambapo wamefanya
maboreso mbalimbali ikiwemo kuwaruhusu wateja wapya kujisajili na kufungua
akaunti zao wenyewe.
Aidha huduma nyingine ni pamoja na uwezo wa kujisajili mwenyewe unaotumia
teknolojia ya AI, muonekano ulioboreshwa kwa mtumiaji, msaada kwa wateja kwa
kutumia AI na sehemu ya maswali na majibu yanayoulizwa mara kwa mara.
“Mchakato wa usajili ni rahisi tu ambapo ni sevu namba ya WhatsApp Banking
iliyothibitishwa ya I&M Banki +255 755 674696 kisha tuma neno habari halafu
fuata maelekezo”, amesema AdamU.
Maeneo ama vipengele muhimu ambavyo vitakuwepo kwenye maboresho hayo
kwaajili ya kurahisisha huduma kwa wateja ni pamoja na, huduma ya Kufungua Akaunti,
ambapo Mteja anaweza kufungua akaunti yeye mwenyewe ndani ya siku moja,
usimamizi wa akaunti ikiwemo kuangalia salio na kupata taarifa za akaunti yake
bure, uhifadhi wa mnufaika, hifadhi kwa urahisi namba ya mnufaika kwaajili ya
kufanya miamala.
Vipengele vingine ni pamoja na kuhamisha Fedha, ambapo mteja anaweza
kuhamisha fedha kwenda akaunti ndani ya benki, kutuma fedha kwenda mitandao ya
simu, kama vile; M-Pesa, Tigo Pesa, Halopesa na Airtel Money, malipo ya bili
mbalimbali, ikiwemo LUKU, DAWASCO, Ving’amuzi nk, kununua muda wa maongezi,
kuchatina mtoa huduma moja kwa moja.
No comments:
Post a Comment