WAZIRI MKUU SERIKALI INA MAHUSIANO MAZURI NA SEKTA BINAFSI, AMPONGEZA MFANYABIASHARA GULAMALI KUFADHILI MAADHIMISHO WIKI YA TPSF, AMPA TUZO YA HESHIMA - UMOJA BANKING BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, 25 July 2024

WAZIRI MKUU SERIKALI INA MAHUSIANO MAZURI NA SEKTA BINAFSI, AMPONGEZA MFANYABIASHARA GULAMALI KUFADHILI MAADHIMISHO WIKI YA TPSF, AMPA TUZO YA HESHIMA

Waziri Mkuu Kasim Majaliwa akimkabidhi Mfanyabiashara Haidary Gulamali Tuzo ya Heshima kwa kuwa mfadhili mkubwa wa Maadhimisho  ya wiki ya Sekta Binafsi (TPSF) 2024,

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema maendeleo yaliyopo nchini hivi sasa yametokana na uhusiano mzuri uliopo baina ya Serikali na sekta binafsi.

“Maendeleo tunayoyaona nchini kwetu katika kila sekta yanategemea mchango wa Serikali pamoja na sekta binafsi. Dhamira na maono ya Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuimarisha sekta binafsi ili ihuishwe na kuwa mshindani katika kuleta maendeleo makubwa kwa nchi yetu,” amesema.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo Julai 23, 2024 wakati akizungumza na wadau wa sekta binafsi nchini kwenye ufunguzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sekta Binafsi Tanzania kwa mwaka 2024 yaliyofanyika Super Dome, Masaki, jijini Dar es Salaam.

Wiki ya Sekta Binafsi Tanzania inaenda sambamba na maadhimisho ya miaka 25 ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Amezitaka wizara na taasisi za Serikali ziendelee kupokea maoni ya sekta binafsi na kuhakikisha yanazingatiwa katika marekebisho ya sera na sheria za biashara ili kuondoa vikwazo vya urasimu na kuboresha taratibu za usajili na uendeshaji wa biashara nchini kwa kuwezesha upatikanaji wa vibali na leseni kwa haraka na kwa urahisi.

Pia amezitaka wizara zinazohusika na viwanda, biashara na uwekezaji zihakikishe zinabuni mbinu za kukuza na kusaidia biashara ndogo na za kati (SMEs). “Wekeni mazingira mazuri ya upatikanaji wa mikopo nafuu, mafunzo na ufikiaji wa masoko ili kusaidia biashara ndogo na za kati kukua na kuchangia katika uchumi. Biashara hizi ni sehemu muhimu ya kuimarisha sekta binafsi.”

Akielezea jitihada ambazo zimechukuliwa ili kukuza sekta binafsi na uwekezaji, Waziri Mkuu amesema Serikali imeimarisha mazingira ya biashara kwa kufanya marekebisho katika sera na sheria za biashara ili kuondoa vikwazo vinavyowakabili wafanyabiashara na wawekezaji.

Mfanyabiashara Haidary Gulamali akizungumza katika maadhimisho hayo alisema licha ya kuzalisha magodoro ya Dodoma Asili pia wanazalisha mafuta ya alizeti ambayo uzalishaji wake kwa siku ni tani 100 na kuwa kiwanda hicho kipo Dodoma.

Alisema kiwanda hicho kimetoa ajili 1000 na wakulima wamepata fursa ya kuuza alizeti katika kiwanda hicho ambapo alihimiza wananchi waendelee kutumia mafuta hayo  bora kwa matumizi ya kupikia vyakula vyao.

Gulamali alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan  kwa kutoa fursa ya kufanya biashara  kwani kampuni yao pia inafanya biashara ya kuagiza vibiriti aina ya kasuku  kutoka nchini Kenya  baada ya kufanya ziara ya kikazi nchini humo.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu na kuomba mfikishie salamu zangu Rais Samia kuwa vibiriti hivi vya kasuku si kwa ajili ya kuwashia jiko tu bali inakwenda kuwasha moto wa miaka mitano mingine tena kwake na kuhakikisha moto huo hautazimika hadi anaingia Ikulu,” alisema Gulamali huku akishangiliwa.

Alisema kwa jitihada za Rais Samia na TPSF waliweza kufanya ziara ya kutembelea Indonesia na wao wakiwa miongoni mwao ambapo alifanikiwa kuleta sabuni ya mche ambayo ameipa jina Gulamali na amehimiza wananchi kudumisha usafi kwa kutumia sabuni hiyo.

Gulamali alisema ziara nyingine kama hiyo waliifanya na Rais Samia  nchini  Norway ambapo walikutana na wafanyabiasha wa nchi hiyo ambapo kampuni yake imeweza kuleta maziwa aina ya Dutch Lady ambayo tayari yapo sokoni hapa nchini na yanachangamkiwa na watanzania pamoja na watalii, bidhaa hiyo ilikuwa ikipatikana katika nchi zao lakini leo hii inapatikana hapa kwetu.

Aidha, Gulamali akisema watanzania wakithubutu wanaweza kwani yeye kupitia kampuni yake ya Gulamali Group of Company wameweza na akatumia nafasi hiyo kuwahimiza wafanyabiasha kulipa kodi kwa ajili ya maendeleo ya nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages