BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imekutana na wateja wake wakubwa yaani makamppuni na taasisi mbali mbali (Corporates) wa jijini Arusha ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya za benki hiyo sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Benki hiyo pia ilitumia fursa hiyo kujadili na wateja hao namna inavyoweza kuboresha huduma zake kulingana na mahitaji yao.



Aidha, kupitia mpango huo benki hiyo imekuwa ikielezea mikakati yake mipana
inayolenga kuwahudumia kwa ufanisi zaidi wateja hao, kuwajengea mitandao ya
kibiashara miongoni mwao sambamba na kuwasogezea huduma za kibenki karibu zaidi
huku huduma ya NBC Connect ikitajwa kama suluhisho muhimu katika kuwasogezea
huduma za kibenki wateja hao wakubwa yakiwemo mashirika na kampuni binafsi,
pamoja na taasisi za serikali.
No comments:
Post a Comment