..........................................
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Hali ya utendaji wa bandari TPA imeboreka ambapo shehena ya
masoko ya nchi jirani iliyohudumiwa kupitia Bandari ya DSM imeongezeka kwa
wastani wa asilimia 8.5 kwa mwaka, kutoka tani milioni 7.8 Mwaka wa Fedha
2021/22 hadi tani milioni 9.2 Mwaka wa Fedha 2023/24.
Kwa upande wa mapato ya Bandari (TPA tariff) yameongezeka
kutoka shilingi trilion 1.1 Mwaka wa Fedha 2021/22 hadi shilingi trilion 1.475
Mwaka wa Fedha 2023/24.
[9:29 PM, 3/3/2025] +255 687 110 880: Tangu Serikali ya
Awamu ya Sita iingie Madarakani hali ya utendaji wa TPA imeboreka ambapo katika
kipindi hiki jumla ya shehena iliyohudumiwa na TPA imekuwa ikiongezeka kwa
wastani wa asilimia 15.23 kwa mwaka kutoka tani milioni 20.78 Mwaka wa Fedha
2021/22 hadi tani milioni 27.55 Mwaka wa Fedha 2023/2024.
Jumla ya shehena iliyohudumiwa katika Bandari ya DSM
iliongezeka kwa wastani wa asilimia 13.38 kwa mwaka kutoka tani milioni 18.67
Mwaka wa Fedha 2021/22 hadi tani milioni 23.98 Mwaka wa Fedha 2023/2024.
Aidha Jumla ya shehena ya Makasha (Containers) iliyohudumiwa
imeongezeka kwa wastani wa asilimia 12.9 kwa mwaka kutoka makasha (TEUs) laki
8.2 Mwaka wa Fedha 2021/22 hadi makasha (TEUs) milioni 1.1 Mwaka wa Fedha
2023/2024.
Kwa Bandari ya Dar es salaam
Jumla ya Shehena ya Makasha iliyohudumiwa katika Bandari ya
DSM imeongezeka kwa wastani wa asilimia 10.7 kwa mwaka kutoka makasha (TEUs)
laki 8.16 Mwaka wa Fedha 2021/22 hadi makasha (TEUs) laki 9.98 Mwaka wa Fedha
2023/2024.
Hayo yanatokana na maboresho makubwa ya Bandari za Tanzania
yaliyofanywa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan
No comments:
Post a Comment