Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi, akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa utoaji huduma kidijitali katika Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Machi 3, 2025 Jijini Dar es Salaam.
............................................
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi amehudhuria hafla ya uzinduzi wa utoaji huduma kidijitali katika Benki ya Taifa ya Biashara(NBC) Jijini Dar es Salaam mgeni rasmi akiwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Majaliwa Kassim Majaliwa .
Katika hotuba yake Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ameishukuru Benki ya NBC kwa namna ilivyochukua hatua ya maendeleo kidijitali hivyo kuiunga mkono Serikali sanjari kukuza uchumi jumuishi ndani na nje ya nchi.
Aidha Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari inatambua jitihada kubwa zinazofanywa na Benki ya NBC kuhakikisha inatoa huduma bora na za haraka kwa wananchi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan alipanua wigo kwa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Ili kuongeza ufanisi kibiahara kwa njia ya kidijitali Kitaifa na Kimataifa kwa kutumia mkongo wa Taifa utakaofikiwa na mikoa yote nchini.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi, akishiriki uzinduzi huo.Taswira ya uzinduzi huo.
No comments:
Post a Comment