Bi. Violet Mordichai, Mjumbe wa Bodi ya Benki ya Stanbic
Tanzania, akipokea cheti kutoka kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu –
Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete, wakati wa
Mahafali ya 10 ya Programu ya Mafunzo ya Mwanamke Kiongozi (Female Future
Program) inayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE). Cheti hiki ni
uthibitisho wa mchango wa Benki ya Stanbic Tanzania katika kufanikisha
programu hii na kuwawezesha wanawake kuboresha ujuzi wao wa uongozi na kushika
nafasi za juu katika sekta mbalimbali. |
Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wanawake
kuvunja vikwazo ili kushiriki katika uchaguzi na kuthibitisha uwezo wao wa
uongozi. Aliwahimiza wanawake kusaidiana na kuchukua majukumu ya dhati katika
kufanya maamuzi. Ujumbe wake ulikuwa wazi kwamba wanawake lazima wainuke,
wachague dhana potofu, na kuunda mustakabali wa Tanzania kupitia uamuzi na
vitendo. Aliyazungumza hayo kwenye mahafali ya kumi (10) ya programu
inayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) iliyofanyika jijini Dar es
salaam.
Kwa upande wake , Violet Mordichai, Mjumbe wa Bodi ya Benki ya Stanbic
Tanzania, aliangazia mipango ya kuwawezesha wanawake katika biashara na
kuwataka wasimamie kazi zao. Pia alisisitiza kuwa uongozi si kusubiri fursa
bali ni kuzitengeneza. Alizungumza hayo wakati anaongea na waandishi wa habari
katika hafla hiyo.
No comments:
Post a Comment