NGOs MSITEMBEE NA FEDHA WEKENI BENKI KWA USALAMA - UMOJA BANKING BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, 22 August 2024

NGOs MSITEMBEE NA FEDHA WEKENI BENKI KWA USALAMA

Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Singida,  Emmanuel Kishosha, akizungumza katika jukwaa la mashirika yasio ya kiserikali (NGOS), Agosti 22, 2024  Mkoa wa Singida.

........................ 


Na Dotto Mwaibale, Singida


WAENDESHAJI wa Mashirika yasio ya Kiserikali (NGOs) Mkoa wa Singida wameombwa kuacha tabia ya kutembea na fedha nyingi wanapokuwa wakifanya shughuli zao kwani kufanya hivyo kunahatarisha usalama wa fedha.


Ombi hilo limetolewa na Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Singida Emmanuel Kishosha wakati akizungumza katika jukwaa la mashirika yasio ya kiserikali (NGOS), Agosti 22, 2024  Mkoa wa Singida.


“ Ndugu zangu niwaombe msitembee na fedha nyingi mnapokuwa kwenye shughuli zenu za kikazi badala yake ziwekeni benki kwa ajili ya usalama kwani benki yetu ya NMB inamatawi kila sehemu mkoani hapa,” alisema Kishosha.


Kishosha alisema mashirika hayo yanaweza kukopesheka na benki hiyo na kuwa wao wanakopesha kuanzia mtu mmoja.


“ Ukitaka kwenda haraka nenda mwenyewe lakini ukitaka kufika  mbali nenda na wenzako,”  alisema Kishosha.


Alisema benki hiyo ipo wazi wakati wote na kama mashirika hayo yatahitaji kupatiwa mafunzo yanayohusu masuala ya kifedha wapo tayari kwani inawataalamu wa kutosha. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages