
…………
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
CHUO cha Benki Mwanza kimemeendela kuwajenga wanafunzi kwenye maadili ili
kuhakikisha wanawapata watendaji wazuri watakaosimamia suala la maadili katika
sekta ya fedha.
Hayo yamebainishwa Leo Agosti 3, 2024 na Bi. Asumpta Muna Mkuu wa Kitengo
cha Mawasiliano Chuo cha Benki Mwanza
Wakati akizungumza na Fullshangwe Blog katika maonesho ya Nanenane
yanayoendelea kufanyika Nzuguni Jijini Dodoma.
Amesema chuo hicho kinamajukumu ya kutoa elimu kwa umma kwa kutoa mafunzo
ya muda mfupi sanjari na sula la maadili.
Ameeleza kuwa mafunzo ya muda mfupi ni kuwajengea uwezo wafanyakazi walioko
kwenye sekta ya fedha ili waendelee kuongeza weledi na ujuzi utakao leta tija
katika kazi zao.
“Kutokana na mafunzo haya kuwa mahili pia yamevutia nchi jirani ikiwemo
Kenya, Uganda, Burundi, Msumbiji,Ghana, Malawi, Zambia hizi ni baadhi ya nchi
ambazo zimekuwa zikileta washiriki kutoka katika benki kuu za nchi hizo kuja
kufanya mafunzo katika Chuo chetu kwa lengo la kuendelea kuwajengea uwezo
wafanyakazi wao”, amesema.
Amesema Chuo hicho kinatoa mafunzo ya muda mrefu katika kozi mbili ikiwemo
astashaada ambayo ni kozi ya miaka miwili na tunachukua wanafunzi ambao
wamemaliza kidato cha sita ambao wana malengo ya kufanya kazi katika sekta ya
fedha.
Aidha, amesema kuwa Chuo hicho kimefungua dirisha la udahili ambao
unaendelea hadi mwezi wa tisa hivyo wanawakaribisha watu wote wanaohitaji
kujiunga kwa ajili ya kufanya udahili.
Wanafunzi waliotembelea banda la Benki Kuu wakipatiwa vipeperushi

Wananchi waliotembelea banda la Benki Kuu wakipatiwa maelezo kuhusu benki hiyo.
No comments:
Post a Comment