UBONGO KUSHIRIKIANA NA VODACOM FOUNDATION NA HOPE INTERNATIONAL KUZINDUA ZIARA MARA NA ARUSHA - UMOJA BANKING BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, 22 July 2024

UBONGO KUSHIRIKIANA NA VODACOM FOUNDATION NA HOPE INTERNATIONAL KUZINDUA ZIARA MARA NA ARUSHA


 .....................................

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

 UBONGO Shirika linaloongoza barani Afrika katika burudani ya elimu kwa watoto, linajivunia kutangaza uzinduzi wa ziara zake za kikanda nchini Tanzania, zinazojulikana kama; "Ziara ya Kujenga Akili," kwa ushirikiano na Vodacom Tanzania Foundation na Hope and Healing International. Ziara ya Kujenga Akili inalenga kutoa uzoefu wa kielimu unaovutia na wenye tija kubwa kwa watoto na walezi kote Tanzania.

Ziara hiyo itaanza katika mikoa ya Mara na Arusha tarehe 15 Julai 2024, ikiwaleta moja kwa moja watoto wahusika wa katuni maarufu barani Afrika na vipindi vya burudani, ikiwa ni pamoja na watoto wenye ulemavu. Iliyoandaliwa ili kuhamasisha kujifunza kupitia michezo, ziara hiyo inatoa mchanganyiko wa kipekee wa elimu na burudani.

"Katika Ubongo, tumejizatiti kutoa maudhui ya kielimu yatakayowezesha viongozi wa kizazi kijacho barani Afrika," alisema Iman Lipumba, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Maendeleo. "Ziara ya Kujenga Akili ni ushahidi wa kujitolea kwetu kufikia watoto katika kila pembe ya nchi ili kuhakikisha wanapata rasilimali na mafanikio.

Basi lenye chapa ya Ubongo litasafiri katika mikoa hiyo, likibeba wahusika wa katuni na waburudishaji kwa ajili ya kufanya maonesho katika shule na vituo vya kijamii.

Vilevile waatashirikisha watoto katika michezo ya kielimu na mashindano huku ziara hiyo ikilenga kujumuisha sherehe za Mwisho wa juma katika kila mkoa ambapo watoto na walezi wao wataweza kushiriki katika shughuli mbalimbali.

Wakati wa sherehe hizi, watoto na walezi watapokea zana maalum zitakazosaidia mchakato wa ujifunzaji.

"Tunafurahi sana kushirikiana na Vodacom Tanzania Foundation na Hope and Healing International katika ziara hii ya kukuza akili. Ushirikiano huu unathibitisha dhamira yetu ya pamoja ya kutoa uzoefu wa kielimu wa hali ya juu kwa watoto na walezi nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages