Akizungumza na wananchi wiilayani Mbinga leo Julai 23, 2024, Kapinga
amesema lengo la serikali ni kuongeza matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia
nchini kutokana na sababu mbalimbali
ikiwemo utunzaji wa mazingira na kuwaepusha wananchi na maradhi yanayotokana na
matumizi ya nishati isiyo safi.
"Hadi sasa kupitia REA tumeshatoa mitungi ya ruzuku 83,500 yenye
thamani ya shilingi bilioni 3.5 na kazi inaendelea." amesema Kapinga.
Ameongeza kuwa, nia ya serikali ni kupunguza gharama za vifaa vya nishati
safi ya kupikia ili wananchi wapate huduma kwa bei nafuu.
Amesisitiza kuwa, serikali inaendelea kufanya mazungumzo na wadau ili
kuongeza Mawakala hadi ngazi ya Vijiji
ikiwemo kutoa ruzuku kwa mawakala hao kupitia miradi mbalimbali.
(hii ni kwa hisani ya gazeti la Nipashe)
No comments:
Post a Comment