CEO WA BENKI YA NMB RUTH ZAIPUNA AFANYA ZIARA KANDA YA MAGHARIBI - UMOJA BANKING BLOG

Breaking

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, 28 July 2024

CEO WA BENKI YA NMB RUTH ZAIPUNA AFANYA ZIARA KANDA YA MAGHARIBI

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bi. Ruth Zaipuna (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa benki hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi Kanda ya Magharibi.

............................... 

Na Mwandishi Wetu

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bi. Ruth Zaipuna, akiambatana na viongozi wengine wa Benki, amefanya ziara ya kikazi katika Kanda ya Magharibi ya Tanzania, ikijumuisha mikoa ya Kigoma, Katavi, Tabora, Simiyu, Shinyanga, na Mwanza.

Katika ziara hiyo ya wiki moja iliyomalizika jana, Bi. Ruth Zaipuna amekutana na wafanyakazi wa Benki ya NMB, wateja, na wadau mbalimbali, akilenga kuimarisha uhusiano na kutoa mwongozo kuhusu utekelezaji wa mikakati ya Benki katika maeneo hayo.

Pamoja na mambo mengine, Bi. Ruth Zaipuna amefanya vikao na viongozi wa baadhi ya mikoa hiyo yenye lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha na kuchangia katika ukuaji wa kiuchumi.

Aidha, ziara hiyo pia ilitoa fursa ya kusikiliza maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau na kudhihirisha dhamira yetu ya kuendelea kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya Watanzania katika ngazi zote.

Ziara hiyo ni muendelezo wa juhudi zetu katika kuhakikisha huduma bora za kifedha zinawafikia Watanzania katika kila kona ya nchi. 

#NMBKaribuYako










 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages